Paroles de la chanson Unaniboo par Mwana Mtule

Chanson manquante pour "Mwana Mtule" ? Proposer les paroles
Proposer une correction des paroles de "Unaniboo"

Paroles de la chanson Unaniboo par Mwana Mtule

Ibilisi mapembe 40 hebu niache
Unapenda mi na Mungu tukosane
Una wivu mbaya wewe ushindwe
Siwezi aminia wewe, wewe ni bure

Nampenda zambe mkweli 
Sio kama wewe mtapeli
Acha kunifuata sijakupa kazi ya ulinzi
Acha kunidanganya hujanifunza mziki

Mbinguni ulishindwa kumpigia Mungu mavocals
Si unataka tufanye collabo tuharibu jameni

Ah ah ah ninakuchukia
Ah ah ah unavyonichukia 
Ah ah ah ninakuchukia
Ah ah ah unavyonichukia 

Unaboo (Shetani) Unaniboo (Shetani)
Unaboo (Shetani) Acha kuniboo (Shetani)
Unaboo (Shetani) Unaniboo (Shetani)
Unaboo (Shetani) Unaniboo (Shetani)

Acha acha kabisa, acha acha kunifuatilia
Acha acha kabisa, acha acha kunifuatilia 

Unanitafutaga maneno kila siku
Nakuonaga kwa umbali shetani
Lakini mimi nakuwaga nimenyamaza chini ya maji
Maana ninalindwa na Mungu Baba
Na ninapelekwa pale pazuri 
Lakini sitaki mambo yako, kaa mbali na mimi

Nikome kome, eeh umenichosha aah
Wewe muovu shetani kila siku kunigongea mlango yangu
Unataka chakula yangu, ni nani aliyekupa ruhusa
Uje kwa maisha yangu wewe, wewe

Leo nakushtaki kwa baba, akuchune chune
Mi nimechoka na wewe unaniumiza bure
Huoni mimi ni mali ya zambe
Wewe unacheza na wembe
We utakatwa, leo nakatwa
Mi nangoja kuona ukikatwa
Unaumiza sana moyo wangu shetani
Kwani mimi nilikukosea nini
Wivu yako peleka huko

Siku ya nyani kufa miti zote huwa zinateleza
Naona kama shetani wee miti leo yako inateleza
Nya nya nya nya... punguza maneno shetani
Unanichoke unaniaffect shetani
Unakosea sana kunifuata fuata
Mimi si mali yako unajidanganya

Unaboo (Shetani) Unaniboo (Shetani)
Unaboo (Shetani) Acha kuniboo (Shetani)
Unaboo (Shetani) Unaniboo (Shetani)
Unaboo (Shetani) Unaniboo (Shetani)

Acha acha kabisa, acha acha kunifuatilia
Acha acha kabisa, acha acha kunifuatilia 

Paroles.net dispose d’un accord de licence de paroles de chansons avec la Société des Editeurs et Auteurs de Musique (SEAM)

Sélection des chansons du moment