Paroles de la chanson Yalah par Mbosso

Chanson manquante pour "Mbosso" ? Proposer les paroles
Proposer une correction des paroles de "Yalah"

Paroles de la chanson Yalah par Mbosso

(Ayolizer)

Nimesadiki ya wahenga
Penzi lina raha yake
Mzigo kwa tenga
Ifaacho mtu chake

Denge nimekatwa ngenga
Ah umate mate
Najinyenga nyenga
Mao mao tate

Huwaga sioni
Ninavyoipanda milima
Ulimi sikioni
Mwili wote wanizizima

Mwenzenu sioni 
Macho mawili yote sina
Tunaanza jikoni
Mpaka varandani twalilima

Yalah! yalah yalah, yalah yalah
Oooh yalah yalah yalah
Penzi limenizidia, yalah yalah
Ni kubwa, yalah yalah
Zito, yalah yalah, yalah yalah

Tungezaliwa zamani
Ningesema penzi togo
Tulinywe kibarazani
Tukitafuna maboga

Nimekipanda uani
Kibustani cha uyoga
Tukishiba biryani
Baby tule mboga mboga

Sasa polisi wa nini?
Nikikosa nikamate wewe
Mahakama ya nini?
Nikikosa nihukumu wewe

Penzi chupa la balindi
Tuligide baby hadi tulewe
Videge shorwe vya nini?
Kifaranga we nibebe mwewe

Huwaga sioni
Ninavyoipanda milima
Ulimi sikioni
Mwili wote wanizizima

Mwenzenu sioni 
Macho mawili yote sina
Tunaanza jikoni
Mpaka varandani twalilima

Yalah! yalah yalah, yalah yalah
Oooh yalah yalah yalah
Penzi limenizidia, yalah yalah
Ni kubwa, yalah yalah
Zito, yalah yalah, yalah yalah

Paroles.net dispose d’un accord de licence de paroles de chansons avec la Société des Editeurs et Auteurs de Musique (SEAM)

Sélection des chansons du moment