Paroles de la chanson Mfamaji par Calvin John

Chanson manquante pour "Calvin John" ? Proposer les paroles
Proposer une correction des paroles de "Mfamaji"

Paroles de la chanson Mfamaji par Calvin John

Oooh ulionyesha mwangaza 
Nilipokuwa kwenye giza
Sikuweza kuona macho yangu yalifunga
Nilitapa tapa kama mfa maji

Ukanifungua macho, ukanifungua moyo
Ukanionyesha yaliyo nizunguka
Kwamba kumbe nina maadui
Nina marafiki wengine wazuri
Na wengine wanafiki

Kilicho chema nitameza
Kilichokibaya nitatema
Umenionyesha eeh..

Umenifungua, macho
Sasa naona, naona
Umenifungua, macho
Sasa naona, naona

Sasa naona, naona
Mazuri mabaya yote, naona

Nikitazama kwa macho ya mwilini
Kuona sioni masikini
Mungu nifungue macho ya rohoni
Nione rafiki wa kweli

Shida yangu aibebe kama ya kwake
Kwenye raha taabu na madhaifu yote
Anifaae kwa dhiki huyo ndiye rafiki
Tena si wa kuhisi ni rafiki halisi

Asiye nikatia tamaa
Tena asiyenirudisha nyuma

Umenifungua, macho
Sasa naona, naona
Umenifungua, macho
Sasa naona, naona

Sasa naona, naona
Mazuri mabaya yote, naona
Sasa naona, naona
Sasa naona, naona

Hakuna siri iliyojificha
Sasa naona 
Hakuna siri chini ya jua

Paroles.net dispose d’un accord de licence de paroles de chansons avec la Société des Editeurs et Auteurs de Musique (SEAM)