Paroles de la chanson Bachela par Queen Darleen

Chanson manquante pour "Queen Darleen" ? Proposer les paroles
Proposer une correction des paroles de "Bachela"

Paroles de la chanson Bachela par Queen Darleen

Eti Lava utaoa lini 
Mbona unazingua?
Wazuri wengi mjini
Wezi wanachukua

We kutwa ubishoo
Nywele kuchange mitindo
Wanakuona wafoo
Kila siku uko single

Moyo wa kupenda sina
Ya nini nijipe homa
Si huyu ni mwana Stamina
Rafiki yake Roma

Si unajua ndoa majaliwa
Nasubiria apange Maulana
Atanitunukia
Bado naula ujana

Ujana maji ya moto 
Utakuunguza(Nitakuunguza)
We pita peku mpoto 
Tutakuuguza

Kwanza kuolewa raha
Oh nah nah wili wili
Ona mume wangu hii spa
Atumiliki wawili wili

Umenikumbusha kule Insta udaku
Wanasema mume umekwara
Ati umefuata hela
Ukakubali kuolewa mitara

Hutanishauri mimi, wakati wangu ndo sasa
Mimi mtoto wa mjini
Kula bila shida chini, acha nile bata 
Nijipe stress za nini?

Bora niwe bachela
Sitaki kujifunga funga, kujibana bana
Niwe bachela, kwanza naona mapenzi
Faida hayana

Bora niwe bachela eh
Huo ni utoto unajidanganya
Niwe bachela
Unayoyafanya mwisho hayana
Bora niwe bachela!

Dada Darleen acha kunichachafya
Uliza kilomkuta Dangote
Sijui kangombana na Tanasha
Ametu-unfollow wote

Mapenzi ya siku hizi
Shemeji Lokole mwongoza umbea
Mkigombana tu kashatizi 
Insta nzima yameshaenea

Ndio maana nimetulia 
Navuta pumzi staki kwenda mbio
Mambo ya kujifanya hodari eti mjuzi
Ujuzi huo kwio

Tukiachana na yote 
Mimi bado sikuungi mkono
Wasafi wote 
Mnaonekana mnapenda ngono(Duu)

Hutanishauri mimi, wakati wangu ndo sasa
Mimi mtoto wa mjini
Kula bila shida chini, acha nile bata 
Nijipe stress za nini?

Bora niwe bachela
Sitaki kujifunga funga, kujibana bana
Niwe bachela, kwanza naona mapenzi
Faida hayana

Bora niwe bachela eh
Huo ni utoto unajidanganya
Niwe bachela
Unayoyafanya mwisho hayana

Mabachela piga kelele(Weee)
Piga kelele moja(Weee)
Kelele mbili(Weee weee)
Piga kelele tatu(Weee...)

Wenye wapenzi piga kelele(Weee)
Walio oa(Weee)
Tulio olewa je?(Weee...)

(Abby Daddy)

Paroles.net dispose d’un accord de licence de paroles de chansons avec la Société des Editeurs et Auteurs de Musique (SEAM)

Sélection des chansons du moment