Paroles de la chanson Pokea par Janet Otieno

Chanson manquante pour "Janet Otieno" ? Proposer les paroles
Proposer une correction des paroles de "Pokea"

Paroles de la chanson Pokea par Janet Otieno

 Pokea shukurani zangu pokea
Pokea shukurani zangu pokea
Pokea shukurani zangu pokea
Pokea shukurani zangu pokea

Machozi yananitoka
Nikiketi chini nifikirie
Umbali nilikotoka 
Hata sijui ni vipi nisimulie(aaah)

Mwema, umekuwa mwema kwangu
Tena umekuwa nguzo yangu wee
Umenifunza subira
Ukanizingira kando na kando

Ah tena wanisikia
Nikianguka waniinua eeeh(aaah)

Sasa mahitaji naweka kando
Sijasahau mema
Na ningependa ujue
Vile moyo unafurahishwa na we

Oooh, maneno yananiishia aah
Umenishangaza kwa matendo yako
Vile wanikumbatia aah
Sina lingine

Lilobakia ni 
Pokea shukurani zangu pokea
Sina budi nikwambie
Pokea shukurani zangu pokea

Kwa uaminifu wako
Pokea shukurani zangu pokea
Kwa matendo yako makuu
Pokea shukurani zangu pokea

Ni wewe ulinifunza 
Ati shida ni mtumwa wangu
Tena ukanifanya
Mwana ndani ya ufalme wako

Neno lako ni taa
Hata kwa giza nimulikiwe
Tena wewe ni jiwe
Nikianguka nishikiliwe

Matendo yako yameninyamazisha
Siwezi laumu
Mkono wako wa kiume
Umenishindia magumu

Eeeh, na kila mara wanikumbuka
Kwa mipango yako miema
Eeeh yale mabaya waniondolea 
Unaniwazia mema

Oooh, maneno yananiishia aah
Umenishangaza kwa matendo yako
Vile wanikumbatia aah
Sina lingine

Lilobakia ni 
Pokea shukurani zangu pokea
Sina budi nikwambie
Pokea shukurani zangu pokea

Kwa uaminifu wako
Pokea shukurani zangu pokea
Kwa matendo yako makuu
Pokea shukurani zangu pokea

Paroles.net dispose d’un accord de licence de paroles de chansons avec la Société des Editeurs et Auteurs de Musique (SEAM)

Sélection des chansons du moment