Paroles de la chanson Binadam par Diamond Platnumz

Chanson manquante pour "Diamond Platnumz" ? Proposer les paroles
Proposer une correction des paroles de "Binadam"

Paroles de la chanson Binadam par Diamond Platnumz

Eyoh…
Yoh I'm back Bob Junior, I'm back
Acha vita ianze
Wamechelewa

Ni we pekee unaejua wangapi binadamu wabaya (wabaya)
Ndugu, rafiki, nani ana roho safi, nani ana roho mbaya (mbaya)
Ni we pekee unaejua wangapi binadamu wabaya
Mola, naomba nilinde niwe na upendo wa dhati
Wote niishi nao sawa

Nilipouanza mziki, mbali na dhiki
Nimekutana na matatizo sana
Sikuwa rafiki, sithaminiki
Bado kidogo mie tu nikate tamaa
Wangu moyo, ulivumilia dharau na masimango mi
Mi wangu moyo, ulivumilia utumwa na manyanyaso di
Yaani nahangaika usiku kucha naambulia patupu
Nilikuwa naumia
Moyoni najipa moyo kesho ntakuwa maarufu
Mwisho wa siku nafulia
Ile nahangaika usiku kucha naambulia patupu
Nilikuwa naumia
Najipa moyo kesho ntakuwa maarufu
Mwisho wa siku nafulia

Ni we pekee unaejua wangapi binadamu wabaya (wabaya)
Ndugu, rafiki, nani ana roho safi, nani ana roho mbaya (mbaya)
Ni we pekee unaejua wangapi binadamu wabaya
Mola, naomba nilinde niwe na upendo wa dhati
Wote niishi nao sawa

Kidogo nakula na mama yangu
Siwezi kuwasahau na ndugu zangu
Upendo popote alipo kwa baba yangu
Japo alinikataa
Aa bata nakulaga mi na rafiki zangu
Tunacheza Reggae na masikini wenzangu
Alazwe pepa peponi na bibi yangu
Mjukuu wake Sanana
Sababu ya ugumu wa maisha
Na maumivu ya mapenzi nikaandika "Kamwambie"
Ndo hapo hustle zikaisha, kabariki Mwenyezi watanzinia wanizimie
Asa hivi kwenye tamasha tu likitajwa jina watu wanashangilia
Wengine furaha inazidi kina hadi kabisa wanalia
Asa hivi kwenye tamasha yaani ikitajwa jina watu wanashangilia
Wengine furaha inazidi kina hadi kabisa wanalia

Ni we pekee unaejua wangapi binadamu wabaya (wabaya)
Ndugu, rafiki, nani ana roho safi, nani ana roho mbaya (mbaya)
Ni we pekee unaejua wangapi binadamu wabaya
Mola, naomba nilinde niwe na upendo wa dhati
Wote niishi nao sawa

Eii tena wabaya sana
Ouu wanakatisha tamaa
Eii uh wabaya
Tena wabaya
Ouu aah
Sana, wabaya sana
Wabaya sana
Mmh wabaya sana

Paroles.net dispose d’un accord de licence de paroles de chansons avec la Société des Editeurs et Auteurs de Musique (SEAM)

Sélection des chansons du moment