Paroles de la chanson Cha Unyonge par Ally Mahaba

Chanson manquante pour "Ally Mahaba" ? Proposer les paroles
Proposer une correction des paroles de "Cha Unyonge"

Paroles de la chanson Cha Unyonge par Ally Mahaba

Umaarufu wako ungeupata wapi
Kama sio mimi kukutangaza
Kujisifu kwako, kutakufikisha wapi
Hio bahari ina mashaza

Usione siongei
Vituko vyako mi naviona
Nyuma sirejei
Ulipopachana nishapashona

Wala sikuongopei
Umejazwa maneno maneno maneno
Kuniacha mimi
Tangu ulipopanda bei
Walitoa meno, meno, meno nje
Kunicheka mimi

Kukuvumilia sana
Ipo siku nitapata pia (Maana)
Sitokung'ang'ania
Huko uliko pashike kiukweli

Kweli umenipatia sana
Nimepotea njia (Maana)
Nilikuaminia ukaniziba macho
Ukanitapeli

Nakuombea ulo naye asikuongopee
Kuja kuachwa utalia sana
Wambeya wambeya waogopee
Watakuponza utalia sana sana sana

Nimeuponza, nimeuponza
Nimeuponza wangu moyo
Nimeuponza, nimeuponza
Nimeuponza wangu moyo

Kinyago nakichonga mwenyewe
Kimenitisha aah
Kama kifaranga kaninyakua mwewe
Nimekwisha aah

Hivyo visnap, mashauzi
Navi emoji vya mdomo upande kunikomoa
Kwenye Whatsapp siulizi
Unatupia vipande pande, vya kuniua

Kuna leo na kesho 
Hao wanaokupa ujasiri
Wa kunisema nisema nisema
Vishindo vina mwisho
Sina pupa unafikiri
Kukujibu mapema mapema mapema

Nije na matarumbeta (Na)
Nikutoege nishai (Na)
Mwishowe si tutateta (Wee)
Sio zangu mimi wee

Unawatuma wacommenti (Na)
Wanichambe kila posti (Na)
Wanakesha kwenye neti (Wee)
Sio zangu mimi wee

Nakuombea ulo naye asikuongopee
Kuja kuachwa utalia sana
Wambeya wambeya waogopee
Watakuponza utalia sana sana sana

Nimeuponza, nimeuponza
Nimeuponza wangu moyo
Nimeuponza, nimeuponza
Nimeuponza wangu moyo

Nimeuponza, nimeuponza
Nimeuponza wangu moyo
Nimeuponza, nimeuponza
Nimeuponza wangu moyo

Paroles.net dispose d’un accord de licence de paroles de chansons avec la Société des Editeurs et Auteurs de Musique (SEAM)

Sélection des chansons du moment