Aller au contenu principal

Paroles de la chanson Hila Zimevunjwa par Bernard Mukasa

Paroles de la chanson Hila Zimevunjwa par

Mungu alipopanga ukombozi
Kusudi kutuosha dhambi hizi
Akakubali kwamba ye'mwenyezi
Afe kifo kibaya kionezi
Mti wakamuwamba kama mwizi
Wakidhani ya kwamba ameshindwa

Amefufuka Bwana na mwokozi
Kazivunja hila za Lusiferi
Katukomboa wana wa mwenyezi
Twaimba ndiyo maana nyimbo nzuri

Mungu akakubali kuonewa
Hakuweka wakili kutetewa
Nguo bila hiari kavuliwa
Kapigwa misumari kazomewa
Akabaki kusali kuombea
Wauaji wapate msamaha

Amefufuka Bwana na mwokozi
Kazivunja hila za Lusiferi
Katukomboa wana wa mwenyezi
Twaimba ndiyo maana nyimbo nzuri

Mungu atufundisha kujitoa
Ya wengi maisha kuokoa
Na anatukumbusha kupokea
Yanayotutisha kumwendea
Tusije kukatisha njema nia
Ili kuyapisha ya dunia

Amefufuka Bwana na mwokozi
Kazivunja hila za Lusiferi
Katukomboa wana wa mwenyezi
Twaimba ndiyo maana nyimbo nzuri

Paroles.net dispose d'un accord de licence de paroles de chansons avec la Société des Editeurs et Auteurs de Musique (SEAM)

Sélection du moment