Paroles de la chanson Kwaru par Zuchu

Chanson manquante pour "Zuchu" ? Proposer les paroles
Proposer une correction des paroles de "Kwaru"

Paroles de la chanson Kwaru par Zuchu

(Ayolizer)

Mmmh aaah aah, mmmh aaah
Aaaah, aah

Roho ingekuwa na macho ungejionea
Moyo haufanyi kificho ukiotea
Mimi kifigiso nacho ungeongea
Mwili wangu rojorojo nanyong'onyea

Chungu nilichopika wamepakua wenzangu
Huruma napokutishwa wamechukua wezangu

Na kitabu chetu cha mapenzi
Kurasa wamechanachana
Hazisomeki tena tenzi 
Vimepoteza maana

Mpofu moyo wangu
Ulishindwa ona
Hukuandikwa wa kwangu
Limenikaba nalitema

Kwaru kwa kwaru kwaru
Kachukua kisu ye anaukwarua
Kwaru kwa kwaru kwaru
Moyo wangu unaumia

Kwaru kwa kwaru kwaru
Ye kwa nguvu anaukwarua 
Kwaru kwa kwaru kwaru
Jamani moyo wangu unaumia

Eeh langu tatizo
Nachuna najimaliza
Mi nakesha kumwaza
Naweweseka lake jina, ooh jina

Oooh basi kwa unyonge 
Najikaza niache kulia
Maana kwake bahati sina, ooh sina

Maumivu ameipora furaha yangu
Oooh amekwenda nayo
Na zangu mbivu zimeniozea
Hasara kwangu, yatapita hayo

Mpofu moyo wangu
Ulishindwa ona
Hukuandikwa wa kwangu
Limenikaba nalitema

Kwaru kwa kwaru kwaru
Kachukua kisu ye anaukwarua
Kwaru kwa kwaru kwaru
Moyo wangu unaumia

Kwaru kwa kwaru kwaru
Ye kwa nguvu anaukwarua 
Kwaru kwa kwaru kwaru
Jamani moyo wangu unaumia

Paroles.net dispose d’un accord de licence de paroles de chansons avec la Société des Editeurs et Auteurs de Musique (SEAM)