Paroles de la chanson Wale Wale par Lava Lava

Chanson manquante pour "Lava Lava" ? Proposer les paroles
Proposer une correction des paroles de "Wale Wale"

Paroles de la chanson Wale Wale par Lava Lava

Naumwa nina maradhi
Nipelekeni hospitalini
Mwenzenu naumwa moyo umekufa ganzi
Nimechoka kunywa quinini

Nahisi ukichaa 
Nusu tahira uchizi
Naona kinyamazongo
Niliyavagaa rambi nikaipiga mbizi
Ikanipasua ubongo (Ubongo)

Angeniambia basi, tungeachana kizungu
Ningempa nafasi, kuliko kutupanga mafungu
Nisinge gasi, japo ni ngumu machungu
Chanya na hasi, yote napanganga Mungu

Kibatari kazidisha tambi, penzi limelipuka
Ye anacheat haogopi dhambi, anaruka ruka
Moyo kaupiga bambi, umeshateuka
Popote anaweka kambi, kutwa nachepuka

Yaani ndo wale wale
Wanaokujaga na tafadhali nakupenda (Wale wale)
Wakimaliza shida zao wanakwenda (Ndo wale wale)
Ati ooh nilipotoka nilitendwa (Wale wale)
Kumbe ni waongo, waongo

Oooh nenda mwambie
Mapenzi hayana jangili yanaumiza
Tena mwambie 
Kuna walo matajiri washalizwa

Usimfiche mwambie
Mapenzi hayana utabiri si miujiza
Fanya mwambie
Mimi si wa kwanza kuumizwa

Yaliwatesa vikongwe 
Tulisoma vitabuni
Nami amenipa mazonge
Najikaza kisabuni

Sawa mimi ni mnyonge
Damu yangu ya kunguni
Mi fungu la tatu ikibonda
Mwezangu lake love me 

Angeniambia basi, tungeachana kizungu
Ningempa nafasi, kuliko kutupanga mafungu
Nisinge gasi, japo ni ngumu machungu
Chanya na hasi, yote napanganga Mungu

Kibatari kazidisha tambi, penzi limelipuka
Ye anacheat haogopi dhambi, anaruka ruka
Moyo kaupiga bambi, umeshateuka
Popote anaweka kambi, kutwa nachepuka

Yaani ndo wale wale
Wanaokujaga na tafadhali nakupenda (Wale wale)
Wakimaliza shida zao wanakwenda (Ndo wale wale)
Ati ooh nilipotoka nilitendwa (Wale wale)
Kumbe ni waongo, waongo

Mwache afanye anachotaka (Hanikomoi, wala hanikomoi)
Sishtuki hata (Hanikomoi, wala hanikomoi)
Sina hofu sina mashaka (Hanikomoi, wala hanikomoi)
Bure anatapa tapa (Hanikomoi, wala hanikomoi)

(The Mix Killer)

Paroles.net dispose d’un accord de licence de paroles de chansons avec la Société des Editeurs et Auteurs de Musique (SEAM)

Sélection des chansons du moment