Paroles de la chanson Sabuni ya Roho par Best Naso

Chanson manquante pour "Best Naso" ? Proposer les paroles
Proposer une correction des paroles de "Sabuni ya Roho"

Paroles de la chanson Sabuni ya Roho par Best Naso

Wanasema kwenye dunia 
Ukiwa na pesa shida
Wanasema kwenye dunia 
Ukiwa na pesa utang'aa

Unaweza fanya lolote
Ukatukana yoyote
Na watu wakasema sawa

Unaweza fanya chochote
Na ukampiga yoyote
Na bado wakasema sawa

Yarabi tustahi
Wake za watu wanasaliti ndoa
Kwa sababu ya pesa

Yarabi tustahi
Ona maskini wanakosa haki
Kwa sababu ya pesa

Miziki tena kanisani wanaiuza dini
Kwa sababu yake pesa
Kwa zaidi ata niliyempenda naye
Amenisaliti

Anasema kachoshwa na shida
Na hivi karibuni anaolewa
Oooh mpenzi ndoa oooh
Sina changu naumia

Oooh pesa, pesa sabuni ya roho
Pesa, pesa sabuni ya roho
Oooh pesa, pesa sabuni ya roho
Pesa, pesa sabuni ya roho

Namuona babu mzee
Anatumikishwa kazi na kijana mdogo
Namuona bibi mzee
Anabebeshwa mizigo na vijana wadogo

Naziona nchi zinapigana
Watu wanarogana eeeh
Kwa sababu ya pesa

Namuona mama anatukanwa
Tena na katoto kadogo
Kwa sababu ya pesa

Mtaani kwetu kuna wazee
Wameoa vibibi vidogo 
Kwa sababu ya pesa

VH wadogo wanazaa
Hakuna anayekataa
Kila kona za mitaa 
Machokoraa wamezagaa

Ona wanaishi vizuri
Wale wenye pesa zao
Magari yao mazuri
Wale wenye pesa zao
Tena wanavaa vizuri
Wale wenye pesa zao
Pesa kiboko kiboko ya njaa

Oooh pesa, pesa sabuni ya roho
Pesa, pesa sabuni ya roho
Oooh pesa, pesa sabuni ya roho
Pesa, pesa sabuni ya roho

Kama pesa zingekuwepo 
Unadhani angekuwepo?
Au zingekuwepo pesa 
Haya yote yangekuwepo?

Hili swali jibu swali
Usiniulize maswali
Kichwa changu kinauma 
Nabaki natafakari

Kama pesa zingekuwepo 
Unadhani angekuwepo?
Au zingekuwepo pesa 
Haya yote yangekuwepo?

Hili swali jibu swali
Usiniulize maswali
Kichwa changu kinauma 
Nabaki natafakari

Paroles.net dispose d’un accord de licence de paroles de chansons avec la Société des Editeurs et Auteurs de Musique (SEAM)

Sélection des chansons du moment