Paroles de la chanson Corona par Beka Flavour

Chanson manquante pour "Beka Flavour" ? Proposer les paroles
Proposer une correction des paroles de "Corona"

Paroles de la chanson Corona par Beka Flavour

(Mafia)

Hili gonjwa ni hatari 
Na tena linaua, ua
Ni tishio duniani 
Nani asiyejua, jua

Kusema za ukweli Corona ni pigo
Mpaka sasa dawa haijulikani bado
Tujilinde wenyewe kwa hili tatizo

Tusipeane mikono chonde chonde
Safari zisomuhimu tusiende
Tuvae mask chafia tuzikinge
Ndio kinga mbadala aah

Mabusu kupigana vyama tusipende
Ili tusiambukizane tujikinge
Mpaka gonjwa hili lipite
Tuombe Mungu atunusuru kwa hili

Tusichukulie tu poa poa 
Corona gonjwa hatari
Watu wanakwisha
Nchi zote duniani

Tusichukulie tu poa poa
Corona gonjwa hatari
Watu wanakwisha
Nchi zote duniani

Na serikali inatupenda 
Ndio maana wamezifunga shule
Mikutano ya kisiasa yote wameitupa kule
Na matamasha wasanii hakuna kule
Wangeruhusu yaani ingekuwa sawasawa na bure

Tunawe mikono kwa maji safi salama
Sanitizer nyumbani no kukosekana
Salamu mbali mbali no Kugusana
Aaaa aaah...
 
Tusipeane mikono chonde chonde
Safari zisomuhimu tusiende
Tuvae mask chafia tuzikinge
Ndio kinga mbadala aah

Mabusu kupigana vyama tusipende
Ili tusiambukizane tujikinge
Mpaka gonjwa hili lipite
Tuombe Mungu atunusuru kwa hili

Tusichukulie tu poa poa
Corona gonjwa hatari
Watu wanakwisha
Nchi zote duniani

Tusichukulie tu poa poa
Corona gonjwa hatari
Watu wanakufa eh
Nchi zote duniani

Bado tunakuomba Mungu Baba
Utunusuru na hili janga
Rais wetu Magufuli baba
Umnusuru na hili janga

Bado tunakuomba Mungu Baba
Utunusuru na hili janga
Ommy mwalimu ooh mama
Umnusuru na hili janga

Bado mi nakuomba Mungu Baba
Uninusuru na hili janga
Mwanangu Ariani
Umnusuru na hili janga eh

Ooh Tanzania 
Utunusuru na hili janga

(Mafia)

Paroles.net dispose d’un accord de licence de paroles de chansons avec la Société des Editeurs et Auteurs de Musique (SEAM)

Sélection des chansons du moment